Online Job Application Portal



MUHIMU: KWA WAOMBAJI WOTE

             
Sifa za Mwombaji
  1. Awe raia wa Tanzania
  2. Awe na umri usiopungua miaka 18 na usiozidi Umri wa miaka 50
  3. Asiwe mwajiriwa wa Serikali au mwajiriwa wa Hospitali za Mashirika ya Dini ambaye mshahara wake unalipwa na Serikali.
  4. Awe na sifa na weledi kwa Mujibu wa Waraka wa Maendeleo ya Utumishi Namba. 1 wa mwaka 2009.
             
Maombi yote yaambatishwe na nyaraka zifuatazo
  1. Nakala ya cheti cha kuzaliwa
  2. Nakala ya Cheti cha Kidato cha Nne/Sita na Stashahada/Shahada kulingana na Kada iliyoainishwa
  3. Kwa aliyesoma nje ya nchi au mitaala ya nje waambatishe cheti cha Ithibati kutoka Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA).
  4. Nakala ya Vyeti vya Taaluma (Cheti na Transcripts). Aidha, waliosoma vyuo vya nje ya Nchi, waambatishe cheti cha Ithibati kutoka TCU
  5. Wasifu (C.V).
  6. Nakala ya cheti cha Usajili/Leseni hai ya taaluma husika (Full Registration/Valid Licence).
  7. Picha ndogo (Passport size) moja ya hivi karibuni.
  8. Nakala ya Kitambulisho cha uraia (NIDA)/Namba ya Utambulisho ya NIDA
  9. Iwapo majina yako yanatofautiana katika vyeti vyako pamoja na Cheti cha kuzaliwa na NIDA hakikisha unawasilisha kiapo cha majina (Deed Pool) kutoka kwa Msajili wa Viapo na kusajiliwa na Msajili wa Hati, Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi
             
Namna ya kuwasilisha maombi
  1. Muda wa kutuma maombi haya ni ndani ya wiki mbili (2) kuanzia tarehe ya kutoka kwa Tangazo hili (Mwisho wa kutuma maombi ni Tarehe 10/02/2023). Maombi yote yawasilishwe kupitia mfumo wa ajira wa Wizara unaopatika kupitia tovuti ajira.moh.go.tz. Waombaji wote mnakumbushwa kuwa makini mnapowasilisha maombi kuhakikisha umejaza vizuri vipengele vyote vinavyotakiwa kwenye mfumo ikiwa ni pamoja na kuambatisha nyaraka zote zinazohitajika.

Kwa maelezo zaidi jinsi ya kutumia mfumo huu pakua maelezo haya Instructions on how to Apply?

Sign In


       
Are you new applicant? Register
       
Forget password?

© 2023 Ministry of health, community development, gender, elderly and children